SHINYANGA HOI AGIZO LA RAIS MAGUFULI

Wanafunzi wa shule ya Msingi Kanawa wilayani Kishapu wakiwakilisha shule ambazo hazijakamilisha utengenezaji wa Madawati mkoani Shinyanga,wakisoma huku wakiwa wamekaa chini ya sakafu na kuiona shule kama jela.

Wanafunzi wakiendelea na Masomo huku migongo ikiwa hoi baada ya shule yao kutokuwa na madawati

SOMA HABARI KWA KINA

Serikali ya mkoa wa Shinyanga imeshindwa kukamilisha agizo la Rais John Magufuli la kutatua tatizo la uhaba wa Madawati kwa shule za msingi na sekondari ambapo bado inakabiliwa na upungufu wa madawati 9,545 

Rais Magufuli alitoa agizo hilo la kukamilisha uhaba wa madawati kwa shule zote nchini ambapo mwisho wa kukabidhi madawati hayo ilipangwa kuwa june 30  huku mkoa wa Shinyanga ukishindwa kutekeleza agizo hilo.

Akitoa takwimu hizo jana Ofisa Elimu taaluma mkoa James Malima amesema  katika shule za msingi kuna upungufu wa madawati 7,310, sekondari 2,235 na kufanya jumla kuu kuwa ni 9,545 huku utengenezaji wa madawati hayo kwenye halimashauri bado ukiendelea ambapo badhi yao zimeshavuka lengo.

Aidha Malima ametaja halmashauri ambazo zimetekeleza agizo hilo la Rais Magufuli la kumaliza tatizo la uhaba wa madawati kuwa ni halmashauri ya mji wa kahama, na msalala,ambazo zImemaliza tatizo hilo kwa shule zote za msingi na sekondari.

Pia Malima amezitaja halmashauri za Ushetu ambayo imekamilisha tatizo la madawati kwa shule za sekondari pekee, huku shule za msingi ikiwa na upungufu wa madawati 387, shinyanga manispaa nayo ikabiliwa na uhaba wa madawati 2,033 kwa shule za msingi ambapo sekondari imeshatekeleza agizo hilo.

Hata hivyo amezitaja halmashauri mbili ambazo hazijatekeleza agizo hilo kwa shule zote kuwa ni kishapu ambapo shule za msingi inakabiliwa na uhaba wa madawati 2,112,sekondari 1,965, Shinyanga vijijini msingi 2,778,sekondari 270 na hivyo kufanya mkoa kuwa na upungufu wa madawati 9,545.

Na Marco Maduhu -Msukuma Blog








Powered by Blogger.