AUA KICHANGA KWA KUKICHIMBIA SHIMONI


Kamanda wa Jeshi la Polisi Mkoani Shinyanga Mika Nyange

SOMA HABARI KAMILI
 
Mwanamke anayefahamika kwa jina la Mariamu Shabani(21) mkazi wa mtaa wa Sango kata ya Nyasubi wilayani Kahama mkoani Shinyanga anashikiliwa na Jeshi la Polisi kwa kosa la Kumuua Mtoto wake Mchanga baada ya kujifungua na Kumchimbia Shimoni.

Tukio hilo limetokea june 18 mwaka huu ambapo mwanamke huyo ni Muhudumu wa baa ya Sosho Mjini Kahama ambaye alijifungulia nyumbani na kisha kuchimba Shimo na kukifukia Kichanga hicho ambacho kiliokolewa na majirani na kukimbizwa hospitali ambapo baada ya Muda mfupi Kilifariki dunia.

Akitoa taarifa kwa vyombo vya habari Mrakibu Mwandamizi wa Jeshi la Polisi mkoani Shinyanga Graphton Mushi kwa niaba ya Kamanda wa Jeshi hilo Mika Nyange, alisema baada ya Kichanga hicho kuokolewa na Majirani na kukimbizwa hospitali ya Wilaya hiyo na kufariki, hivyo mzazi huyo anashitakiwa kwa kosa la Mauji.

Mushi alisema Mwanamke huyo hivi sasa yupo chini ya Jeshi hilo na anatarajiwa kufikishwa Mahakamani kujibu Shitaka linalomkabili la Mauji ililiwe fundisho kwa wazazi wengine wenye tabia kama hiyo, na kukomesha Matukio ya kikatili mkoani Shinyanga. ambayo yameonekana kushika kasi.

Katika tukio jingine Jeshi la Polisi linamshikilia Mwanaume Balele Zanzibar mkazi wa Songwa kata ya Mwigumbi Wilayani Kishapu kwa kosa la Kumuodhesha Mtoto wake ambaye ni  Mwanafunzi wa darasa la Sita  Unisi Balele kwa kupokea Ng’ombe 14 na kumuachisha Masomo yake.

Akielezea tukio hilo Kamanda Mushi alisema zoezi la kutimbua ndoa hiyo na kumkamata Mzazi huyo na Muoaji lilifanyika june 18 kwa kushirikiana na Shirika la kutetea haki za watoto Agape ambao ndio walitoa taarifa kwa Jeshi hilo na kufika eneo la tukio na kukuta ndoa ya Kimila ikifungwa na kufanikiwa kuwa kamata wahusika wote.

“Baada ya kufika eneo la tukio tulikuta ndoa ya Kimila ikifungwa na hivyo kuwakamata Baba wa mtoto, na  Muoaji ambaye ni Sena Sungwa mkazi wa Maswa Simiyu kwa kosa la kuodhesha na Kuoa Mwanafunzi wa darasa la Sita jambo ambalo ni kosa Kisheria,”alisema Mushi

Aidha Mushi alisema watuhumiwa wote wanatarajiwa kufikishwa Mahakamani ilikujibu Shitaka linalo wakabili na kupewa adhabu kali ya Kisheria, huku akitoa wito kwa wazazi na walezi mkoani Shinyanga kuacha tabia ya kuthamini Mifugo na kukatisha Ndoto za watoto wao kwa kuwaodhesha wakiwa na umri mdogo

Na Marco Maduhu -Shinyanga
 
Powered by Blogger.