VETA SHINYANGA YAZINDUA MAFUNZO MAPYA YA UPATIKANAJI WA AJIRA MIGODINI,TANROAD

 

Barozi wa Canada nchini Tanzania  Nathalie Garon Mkono wa kushoto akikata utepe wa kuzindua mafunzo mapya ya utengenezaji wa mitambo mikubwa (Heavy duty Equipment Mechanics Work Shop) katika chuo cha Veta mkoani Shinyanga akiwa na  mkurugenzi wa elimu ya ufundi na mafunzo ya ufundi Stadi kutoka wizara ya ya elimu sayansi na tecknolojia Mhandisi Thomas Katebalirwe mkono wa kulia.


SOMA HABARI KAMILI


Chuo cha ufunzi stadi Veta mkoani Shinyanga, kimezindua mafunzo mapya ya utengenezaji wa mitambo mikubwa (heavy duty equipment mechanics work shop)  ambayo yatasaidia vijana wengi kupata ajira kwa urahisi ndani ya Migodi na Tanroad sababu mafundi wa mitambo hiyo wapo wachache hapa nchini.

Zoezi la uzinduzi wa mafunzo hayo mapya (Course mpya) limefanyika februari 19 mwaka huu chuoni hapo, ambapo vifaa vya mafunzo ya utengenezaji wa mitambo hiyo yakiwa yamefadhiliwa na Serikali ya Canada, kwa mlengo wa Serikali ya Tanzania kuongeza idadi kubwa ya wataalamu wake ndani ya nchi, kwa kupata mafundi wa mitambo hiyo pamoja na kupunguza tatizo la ajira kwa vijana.

Akizungumza kwenye uzinduzi wa Course hiyo mpya mkuu wa chuo cha Veta mkoani Shinyanga Afridon Mkhomoi, alisema baada ya kuona mkoa wa Shinyanga umezungukwa na migodi mingi, na wanapokuwa wakipeleka vijana wao kufanya kazi kwa vitendo kwenye migodi hiyo, wamekuwa wakipokea chagamoto ya kwanini wasiwe na course ya utengenezaji wa mitambo chuoni hapo ambayo itawasaidia vijana wengi kupata ajira kwa urahisi ,na hivyo kuamua kuanza mchakato wa kuianzisha na hatimaye wamekamilisha.

Alisema baada ya kupokea changamoto hiyo, ndipo wakapata ufadhili wa vyuo vya Veta kutoka nchini Canada kwa kupewa vifaa hivyo vya mafunzo ya utengenezaji wa mitambo mikubwa, na mpaka sasa wamesha dahili wanafunzi 20 ,wakike wakiwa Wanne  na wakiume 16,na usomaji wake utachukua Miaka Mitatu, na kubainisha Mwanafunzi kama akifikisha miaka miwili pia anaweza kwenda kufanya kazi, huku akimalizia mwaka wake wa mwisho polepole.

“Natoa wito kwa vijana mkoani Shinyanga kuichangamkia Course hii mpya ambayo itawapatia ajira kwa urahisi ndani ya migodi kwa kutengeneza mitambo ambayo itakuwa ikiharibika sababu wataalamu wake ni wachache,” alisema.

Naye Kaimu mkurugenzi wa masoko mipango na maendeleo kutoka  Veta makao makuu  Hildegardis  Bitegera, akimwakilisha  kaimu mkurugenzi wa Veta kutoka makao makuu Dk Ndazi Bwile, aliwataka vijana wanaosoma mafunzo hayo wawe na bidii ya kusoma ikiwa fani hiyo inafaida kwenye soko la Ajira .

Kwa upande wake mkurugenzi wa elimu ya ufundi na mafunzo ya ufundi Stadi kutoka wizara ya ya elimu sayansi na tecknolojia Mhandisi Thomas Katebalirwe, alisema wao kama wizara walipitisha mafunzo hayo tangu mwaka 2015, na matarajio ya Serikali katika Course hiyo mpya ni kupata watalamu wengi hapa nchini wa Mitambo hiyo.

Aidha Meneja wa mradi  wa vifaa vya kutengenezea mitambo hiyo kutoka nchini Canada katika chuo cha College of New Colidonia (CNC)Romana Pasca, alisema wameamua kufadhili vifaa hivyo ili tanzania ipate  kuongeza idadi kubwa ya wataalamu wake ndani ya nchi wa kutengeneza mitambo, pamoja na kupunguza tatizo la ajira kwa vijana.

Nao baadhi ya wanafunzi wanaosoma mafunzo hayo mapya akiwamo Calvin Msafiri, waliipongeza Serikali kwa kushirikiana na nchi ya Canada kuanzisha Course hiyo mpya ambayo itawapatia ajira kwa urahisi na kuinua uchumi wa maisha yao.

SOMA PIA HABARI PICHA HAPA CHINI


 Mkuu wa chuo cha Veta mkoani Shinyanga Afridoni Mkhomoi akisoma taarifa ya chuo hicho juu ya mafunzo hayo mapya ya utengenezaji wa mitambo mikubwa, na kuishukuru Serikali ya Canada na chuo cha College of New Colidonia (CNC) kwa ufadhili walioutoa wa vifaa hivyo vya kujifunzia kutengenezea mitambo hiyo ambayo itatoa fursa kubwa ya vijana kupata ajira hasa migodini na Tanroad.
 Kaimu mkurugenzi wa masoko mipango na maendeleo kutoka  Veta makao makuu  Hildegardis  Bitegera, akimwakilisha  kaimu mkurugenzi wa Veta kutoka makao makuu Dk Ndazi Bwile, akiwataka vijana wanaosoma mafunzo hayo ya utengenezaji wa mitambo mikubwa, wawe na bidii ya kusoma ikiwa fani hiyo inafaida kwenye soko la Ajira .

 
mkurugenzi wa elimu ya ufundi na mafunzo ya ufundi Stadi kutoka wizara ya ya elimu sayansi na tecknolojia Mhandisi Thomas Katebalirwe, akizungumza kwenye uzinduzi wa mafunzo hayo mapya, na kusema kuwa serikali inatarajia matokeo makubwa ya kupata wataalamu wake wengi wa ndani ya nchi wa kutengeneza mitambo hiyo mikubwa.

Meneja wa mradi  wa vifaa vya kutengenezea mitambo hiyo kutoka nchini Canada katika chuo cha College of New Colidonia Romana Pasca, akizungumza kwenye uzinduzi wa mafunzo hayo mapya na kusema wameamua kufadhili vifaa hivyo ili tanzania ipate  kuongeza idadi kubwa ya wataalamu wake ndani ya nchi wa kutengeneza mitambo mikubwa pamoja na kupunguza tatizo la ajira kwa vijana.

mjumbe wa bodi wa chuo hicho cha Veta mkoani Shinyanga  Elias Kasitila, ambaye pia ni  meneja wa Acacia wa kampuni ya uchimbaji madini ya dhahabu Buzwagi, akiwataka vijana wanaosoma chuoni hapo kujenga tabia ya kujiajiri wenyewe na wasiwe na dhana ya kuwa wote wata ajiriwa ikiwa pale watakapohitimu mafunzo yao, ambapo tayari wanakuwa na ujuzi ambao wata utumia kuwa ingizia kipato pamoja na kuweza kuunda vikundi vya ujasiriamali, na kupata mikopo ambayo itawasaidia kuanzisha hata viwanda vyao na kuwaingizia kipato kizuri na kuendesha maisha yao bila shida.

 
Baadhi ya vifaa ambavyo vijana watakuwa wakijifunzia kutengeneza mitambo mikubwa katika mafunzo hayo mapya ya heavy duty equipment mechanics work shop.

Wageni waalikwa na wakufunzi wa chuo hicho wakiangalia vifaa vya kujifunzia namna ya kutengeneza mitambo mikubwa, ambavyo vimefadhiliwa na Serikali ya Canada kupitia chuo cha  College of New Colidonia (CNC).

 
Baadhi ya mitambo ambayo wanafunzi wa chuo hicho cha Veta mkoani Shinyanga ambayo hujifunzia kutengeneza barabara.
 Mwalimu wa Library  Ezekiel Joachimu kutoa chuo cha Veta mkoani Shinyanga mkono wa kulia akimuonyesha vitabu vya mafunzo ambavyo husomea wanachuo wa Veta  Dkt Alan Copeland ambaye ni mshauri mkuu wa taasisi ya Cican ya Canada inayotekeleza mradi wa Istep.
 Mshauri mkuu wa taasisi ya Cican ya Canada inayotekeleza mradi wa Istep Dkt Alan Copeland, akiwa na mwalimu wa Library kutoka chuo cha Veta mkoani Shinyanga Ezekiel Joachimu ,wakiwa katika Library ya vitabu chuoni hap0.
 
 Mwalimu wa mafunzo ya ukataji wa madini ya Vito na ung'alishaji Yona Mwambopa, akielezea namna wanafunzi chuoni hapo wanavyojifunza mafunzo hayo ambayo pia yatawapatia ajira migodini kwa urahisi.
Baadhi ya Vifaa ambavyo hujifunzia wanafunzi wa chuo cha ufundi Veta mkoani Shinyanga, namna ya kukata na kug'arisha madini hayo ya Vito.
 Baadhi ya wageni waalikwa kwenye uzinduzi wa mafunzo hayo mapya ya kutengeneza mitambo mikubwa katika chuo cha Veta mkoani Shinyanga ,wakiangalia namna madini hayo ya vito jinsi yalivyokatwa kitaalamu pamoja na kung'arishwa.
 Muonekano wa madini hayo ya Vito yakiwa tayari yameshakatwa na Kung'arishwa kama unavyo yaona ambayo baadhi yake ni Amethyst, Quart, Tourmaline, Agate a Citrinr.
 Mwanachuo cha Veta mkoani Shinyanga akitoa burudani ya kuruka sarakasi kwenye hafla fupi ya uzinduzi wa mafunzo mapya ya utengenezaji wa mitambo mikubwa  Heavy Duty Equipmet Mechanics work Shop.
 Mwanafunzi wa Veta, Mkapa Malijani anayesoma fani ya Computer and Secretary akielezea wageni waalikwa namna wanavyosoma fani hiyo.


 Baadhi ya wanafunzi wa chuo cha Veta wanaosoma Fani ya Computer and Secretary chuoni hapo.

 Mshauri mkuu wa taasisi ya Cican ya Canada inayotekeleza mradi wa Istep Dkt Alan Copelanda akiahidi kuendelea kushirikiana na chuo hicho cha Veta mkoani Shinyanga katika suala zima la kuboresha mafunzo ambayo yatawapatia ajira vijana.

Wanafunzi wa chuo cha Veta wakiendelea kutoa burudani.
 wanafunzi wa chuo cha Veta wakisikiliza Nasaha mbalimbali kutoka kwa wageni waalikwa ikiwamo ya kujenga dhana ya kujiajiri wenyewe ikiwa ujuzi wanao wa kufanya kazi na kuwaingizia kipato
Baadhi ya wanafunzi wa chuo cha Veta Shinyanga wakiwa wamevaa Tshit ya chuo cha College of New Colidonia (CNC) ambacho ndicho kimefadhili vifaa hivyo vya kujifunzia kutengeneza mitambo mikubwa.
 Tunasikiliza Nasaha mbalimbali kutoka kwa wageni waalikwa
 wanafunzi wa chuo cha Veta Shinyanga wakiwa makini kuyashika yale wanayoambiwa na wageni waalikwa namna ya kutumia ujuzi wao wanaoupata kuwaingizia kipato na kuendesha maisha yao bila hata ya kutegemea kuajiriwa.


 
wafadhili wa vifaa  vya mafunzo ya kujifunzia utengenezaji wa mitambo mikubwa kutoka nchini Canada, wakiwa na wageni waalikwa pamoja na viongozi wa chuo cha Veta Shinyanga na makao makuu, pamoja na baadhi ya wanafunzi wa chuo hicho wakiwa katika picha ya pamoja.

Na Marco Maduhu ambaye pia ni Mwandishi wa Gazeti kubwa hapa nchini la Nipashe soma kila siku Gazeti lako pendwa uhabalike.



Powered by Blogger.