WANANCHI WAMFUNGIA BARABARA MKANDARASI KWA MAGOGO,MAWE

Wananchi wa Kata ya Masekelo wa Manispaa ya Shinyanga wakiwa wamefunga barabara kumzuia Mkandarasi wa Kampuni ya Jasco inayosomba Moramu kutoka kwenye eneo hilo na kupeleka Mjini Shinyanga kwenye utengenezaji wa barabara kwa kiwango cha Lami, ambapo Magari ya Kampuni hiyo yamekuwa yakitimua Vumbi kali kwenye Makazi yao pamoja na kukimbia Mwendo Kasi hali ambayo imewafanya kuzui hadi pale watakapo hakikishiwa usalama wao na Magari hayo kutokimbizwa kwa mwendo kasi.
Wananchi wakiwa wamefunga barabara na kuzui Magari hayo kutoendelea na Shughuli za Usombaji Moramu hadi pale barabara hilo litakapo tengenezwa pamoja na kumwagiliwa Maji Mda wote ilikuondoa Vumbi hilo na kuokoa Afya zao ikiwa baadhi yao Tayari wameshapatwa na Magonjwa ya Kikohozi na Kifua, huku akihofia kuuawa sababu ya Magari hayo kukimbia Mwendo kasi .

Mgomo ukiendelea huku Jeshi la Polisi Likiimarisha Ulinzi na Usalama.


Mgomo Ukiendelea
Mkurugenzi wa halmashauri ya Manispaa ya Shinyanga Katikati Mwenye Shati la Kitenge akiongea na Wananchi wa kata hiyo ya Masekelo na kutafuta Suluhu ya kuruhusu Magari hayo kuendelea Kufanya kazi za ujenzi wa taifa huku akiahidi suala lao kutatuliwa, na Wakwanza Kushoto Mwenye Miwani ni Mhandisi Mkuu wa Kampuni ya JASCOVasanth Kumar naye akisikiliza maelekezo ya Mkurugenzi ya kutekeleza Mashariti wanayotaka Wananchi ya kuondolewa Vumbi na Mwendokasi

Wakwanza kushotoni Mhandisi mkuu wa Kampuni y JASCO Vasanth Kumar akizungumza na Diwani wa kata ya Masekelo Samweli Sambayi kutafuta Suluhu ya kuondoa Mgogoro huo ,ambapo Suluhu ilipatikana na hatimaye Mgari hayo yakaruhusiwa kufanya Kazi yake kwa Mashariti kwanza ya Kutengeneza Barabara na Kumwagilia Maji muda wote.



SOMA HABARI KWA KINA

Wananchi wa kata ya Masekelo Manispaa ya Shinyanga wamemzuia mkandarasi anayesomba Moramu kwenye eneo hilo (JASCO) kwa kufunga barabara kwa Magogo,Miti, Kamba na Mawe ilikumzuia asiendelee na Shughuli hiyo kwa madai ya kutishia usalama wa Maisha yao baada ya Magari yake kukimbia kwa mwendo kasi na kutimua vumbi kali kwenye makazi yao.

Tukio hilo limetokea jana majira ya Saa moja asubuhi ambapo wananchi hao wakishilikiana na viongozi wao akiwamo diwani wa kata hiyo Samweli Sambayi walifunga barabara hiyo ndani ya Masaa Sita, huku wakizuia Magari ya Mkandarasi huyo yasifanye shughuli ya kusomba Moramu mpaka pale watakapo hakikishiwa usalama wao.

Wakizungumza na Waandishi kwenye tukio hilo baadhi ya Wananchi hao Asha Rajabu, Emmanuel Masanja na Salu Nkwabi walisema Magari ya Mkandarasi huyo yamekuwa yakitimua Vumbi  Kali kwenye Mkazi yao huku yakikimbia Mwendo Kasi hali iliyowalazimu kuifunga barabara hiyo. 

Masanja alisema Magari ya Mkandarasi huyo yamekuwa kero kwenye eneo lao ambayo yanasomba Moramu na kupelekea Mjini Kwenye ujenzi wa barabara za Lami km 13, lakini kutokana na vumbi hilo Tayari wameshaanza kupatwa na Magonjwa ya Kikohozi kisicho Isha  Kuugua Kifua pamoja na kuhofia maisha yao kwa kugongwa na Magari.

“Tunachotaka sisi huyu Mkandarasi Jasco atengeneze kwanza barabara hili kwa kulikwangua pamoja na kumwaga Maji mara kwa mara ilikupunguza vumbi litatumaliza, 
pamoja na Madereva wake wapunguze Mwendo kasi wa Magari ilikunusuru maisha yetu,”alisema  Masanja

Naye Diwani wa Kata hiyo ya Masekelo Samweli Sambayi alisema wameamua Kufunga barabara hiyo ilitatizo lao litatuliwe haraka sababu wameshapeleka Malalamiko yao kwenye uongozi wa halmashauri na Mkandarasi huyo, lakini wamepuuzia na kuendelea kutishia usalama wa maisha ya wananchi wake.

Kwa upande wake Mhandisi Mkuu wa Kampuni ya Jasco inayosomba Moramu kwenye Kata hiyo Vasanth Kumar, alikiri Malalamiko hayo Kuyafahamu huku akianza ukarabati wa barabara hiyo mara moja nakuahidi kulimwagia maji muda wote pamoja na kuwazuia Madereva wake kutoendesha Magari kwa Mwendo Kasi.

Na Marco Maduhu, Msukuma Blog
Powered by Blogger.