RAIS MAGUFULI ATOA ZAWADI YA CHAKULA KAMBI YA WAZEE KOLANDOTO SHINYANGA

Katibu tawala wa mkoa wa Shinyanga Albert Msovela akikabidhi mbuzi wawili na chakula mchele kilo 100 na mafuta ya kupikia lita 20 kwenye kambi ya kulea wazee wasiojiweza iliyopo kolandoto mjini shinyanga kwa ajiri ya kusheherekea sikukuu ya Eid el Fitri  kwa niaba ya Rais Magufuli ambaye ndiye aliyetuma zawadi hizo wapelekewe wazee hao.

Afisa mfawidhi wa kambi hiyo ya wazee wasiojiweza Sophia Kang'ombe akimpokea Afisa tawala wa mkoa Albert Msovela na kupokea zawadi hizo kwa ajiri ya wazee hao kufurahia sikukuu hiyo ya Eid El Fitri kwa kula chakula kama watu wengine walioko majumbani mwao.

Katibu tawala Albert Msovela akizungumza kwenye kambi hiyo ya wazee huku akiahidi serikali kuendelea kuwatatulia changamoto ambazo zinawakabili ikiwa baadhi yao zimefanyiwa kazi kama vile kuwepo kwa maji safi na salama, umeme kufungwa pamoja na kupatiwa matibabu kwa kiwango kizuri huku pia wakifanyiwa utaratibu wa kupata kadi ya bima ya afya.
Mwenyekiti wa kambi hiyo ya wazee (kolandoto) Samweli Maganga akipokea zawadi hiyo ya chakula na kitoweo huku akimshukuru Rais Magufuli kwa kuthamini makundi maalumu, ambapo pia alimuombea aishi maisha marefu yenye mibaraka na afya tele maana ni mtu aliyeletwa na mwenyezi mungu kuwakomboa watu wanyonge ambao walikuwa wamesahaurika kwa miaka mingi
HABARI KWA KINA 

Kambi hiyo inalea wazee 23 pamoja na watoto wao, ambapo wamekuwa wakikabiliwa na changamoto mbalimbali ikiwamo moja kubwa ya ubovu wa majengo, ambayo baadhi yao yamesha anza kuanguka menyewe sababu ya kuchakaa na hivyo kuhofia usalama wa maisha yao.

Akizungumza kambini hapo mwenyekiti wa wazee hao Samweli Maganga mara baada ya kupokea zawadi hiyo ya chakula, alisema anampongeza Rais Magufuli kwa kujali makundi maalumu, huku akiiomba serikali pia iwatatulie tatizo la ujenzi wa majengo mapya ikiwa yaliyopo yamesha choka.

“Tunaipongeza serikali ya awamu ya tano chini ya rais Magufuli hasa kwa kujali makundi maalumu kwa kututatulia changamoto zetu, ikiwa baadhi zimeshatatuliwa ambapo tumefungiwa umeme, maji yapo na suala la matibabu hatupati shida kama zamani, na kero hii ya majengo mabovu tuna amini itatatuliwa tu,”alisema Maganga

Aliongeza” kutokana na utendaji kazi anaouonyesha Magufuli tunamuombea kwa mwenyezi mungu aendelee kuinyoosha nchini katika uimara wake na aiishi maisha marefu bila hata ya kupata maradhi wala vikwanzo maana ni mkombozi wa watu wanyonge.”

Aidha akikabidhi chakula hicho kwa niamba ya Rais Magufuli katibu tawala la mkoa wa Shinyanga Albert Msovela, alisema wametoa mchele kilo 100, mafuta lita 20 pamoja na mbuzi wawili, huku akiahidi serikali kuendelea kuzitatua changamoto moja baada ya nyingine ilikuhakikisha wazee hao wanaishi mahari salama.

Naye mganga mkuu wa mkoa wa Shinyanga dkt Ntuli Kapologwe ambaye aliambatana na katibu tawala huyo kukabidhi zawadi hizo za chakula kambini hapo, alisema pia serikali itafanya mkakati wa kuhakikisha wazee hao wanapatiwa kadi za bima ya afya ambazo zitawasaidia pia kupata matibabu kwa urahisi.

Na Marco Maduhu- Msukuma Blog






Powered by Blogger.