Mkuu wa mkoa mpya wa Shinyanga Zainabu Tareck
SOMA HABARI KWA KINA
Mkuu wa mkoa wa
shinyanga Zainabu Tareck ameskikitishwa na mkoa huo kuwa nyuma kimaendeleo huku
wananchi wake wakikabiliwa na hali ya umaskini licha ya kuzungukwa na rasilimali
nyingi, zikiwamo dhahabu, almasi na viwanda hali ambayo imemlazimu kuwaagiza wakuu
wa wilaya kufanya kazi ya kuuinua kiuchumi.
Tareck
amezungumza hayo july 4 mara baada ya kumaliza zoezi la kuwa apisha wakuu hao wa wilaya
ambao ni Nyambonga Taraba (Kishapu), Fadhili Nkulu (Kahama) na Josephine Matiro
(Shinyanga), na kuwataka wafanye kazi kwa kujituma ilikuuletea maendeleo mkoa
wa shinyanga na kutatua kero za wananchi.
Alisema ni jambo
la kusikitika na kushaghaza mkoa kama wa shinyanga ambao unasifika kuwa na
rasilimali nyingi za madini ya dhahabu na almasi, lakini umedumaa kimaendeleo
huku wananchi wake wakiwa maskini, kitendo ambacho amekipinga na kuahidi
kuubadilisha kuwa kama jiji la madini.
“Haiwezekani
mkoa kama huu wenye madini chungu nzima harafu unakuwa nyuma kimaendeleo, hivyo
naomba na kuagiza wakuu wote wa wilaya na watendaji wa serikali tufanye kazi
kwa juhudi zote ilituubadilishe mkoa wa shinyanga uonekane kama mji kweli wenye
madini.”alisema Tareck
Aidha mkuu huyo
wa mkoa pia aliwagiza wakuu hao wa wilaya wafanyekazi ya kurudisha heshima ya
zao la pamba, ambalo limeonekana kupotea ikiwa zao hilo kwa asilimia kubwa ndio
lilikuwa mkombozi wa mkulima kumuinua kichumi kwa kutatua kero zote
zinazowakabili wakulima.
Nao wakuu hao wa
wilaya watatu wakizungumza mara
baada kula kiapo walimwahidi mkuu huyo wa mkoa
sanjari na Rais John Magufuli, kutowaangusha kwa kuhakikisha wanafanyakazi ya
kuwaletea maendeleo wananchi pamoja na kumalizia tatizo la uhaba wa madawati na
kuendelea kufichua watumishi hewa.
Na Marco Maduhu- Msukuma Blog
|