SHULE YAFUNGWA KUNUSURU VIFO YA WANAFUNZI 900

Mmoja wa wanafunzi wa shule ya msingi bugoyi 'B John Boniface akichungulia kwenye choo cha shule hiyo wakati alipotaka kujisaidia na kuogopa kutumbukia na hivyo kuamua kujisaidia nyuma ya uzio wa shule ilikunusuru maisha yake mara baada ya bampa la choo kutumbukia ambapo choo hicho chenye matundu manane kilijengwa bila nondo kwa usimamizi wa wahandisi wa halmashauri ya manispaa ya shinyanga.'

Moja ya tundu la choo likiwakilisha matundu mengine Manane ambayo yamezungushiwa miba kutoendelea kutumika baada ya bampa kuachia na kutumbukia jambo ambalo ni hatari  kwa maisha ya wananfunzi wawapo shuleni kwao.

Wanafunzi wa shule ya msingi bugoyi B wakiwa eneo la vyoo vya shule hiyo pamoja na baadhi ya wazazi wao kama unavyoona wakitahamaki jinsi wanavyohatarisha usalama wa maisha yao .

Wanafunzi wakishindwa kuendelea na masomo ya na kuzagaa ovyo shuleni mara baada ya kukosa mahari pa kujisaidia huku muda mwingine wakichangia choo kimoja na walimu wao ambacho kipo salama , nacho kikiwa hakikidhi mahitaji ya wanafunzi 909 huku walimu wakiwa 25. na hivyo kuwepo hatari ya kufaniana chooni.

Wazazi nao wakishuhudia matundu hayo ya vyoo vya shule jinsi vinavyo hatarisha maisha ya watoto wao na hivyo kuridhia agizo la idara ya afya ya kata kuifunga shule hiyo hadi pale ujenzi wa matundu mapya ya vyoo vitakapo kamilika kujengwa.

Wazazi wakiendelea na ukaguzi wa vyoo vya shule ambavyo vishatitia na muda wowote vinaweza kuaguka baada ya kujengwa chini ya kiwango.
Hapa ni Mwenyekiti wa mtaa wa mbuyuni kata ya ndembezi Abdala Sube akifungua kikao cha wazazi juu ya kujadili mstakabali wa vyoo hivyo na kunusuru maisha ya watoto wao.

Afisa elimu wa shule za msingi manispaa ya shinyanga Yesse Kanyuma akiomba radhi wazazi mara baada ya kuharibu hali ya hewa kwa kutoa kauli tata kwao na kuwalazimisha wachimbe kwanza shimo la choo ndipo halmashauri itoe pesa ya ujenzi lasivyo hakuna kitakachoendelea, kauli ambayo wazazi waliipinga na kudai kuwa  choo hicho kilicho anguka walichanga pesa zao na kusimamiwa na halmashauri lakini wahandisi wakachakachua pesa zao na kujenga chini ya kiwango, na kudai kuwa kutokana uzembe huo kufanywa na halmashauri hivyo wao wananchi hawatachangia bali halimashauri ndio ihusike na ujenzi huo iliifidishie pesa walizochakachua kwa wananchi.
Aliyesimama ni Diwani wa kata ya Ndembezi David Nkulila akituliza mzuka wa wazazi wawe wapole ilikujadili hatima ya choo hicho.
Kikao kiliendelea huku wawazi wakigeuka mbongo na kutokubali kutoa pesa zingine za ujenzi wa choo hicho kutokana na hapo awali pesa zao kuchezewa na kujengwa choo chini ya kiwango na mzigo huo kuiachia halmashauri.
Wazazi wakisikiliza neno kutoka kwa viongozi wao na hivyo kuridhia shule hiyo ifungwe hadi pale ujenzi wa choo utakapo kamilika ilikunusuru maisha ya watoto wao
SOMA HABARI KAMILI

Shule ya msingi bugoyi “B” iliyopo kata ya ndembezi manispaa ya Shinyanga imefungwa na idara ya afya  baada ya vyoo vyake kutitia na kuhatarisha maisha ya wanafunzi 909  kwa kufukiwa wakati wakijisaidia.

Siku ya jumatatu shule zote hapa nchini zilifunguliwa baada ya likizo ya mwezi wa sita, lakini zimepita siku mbili shule hiyo ya bugoyi imefungwa na wanafunzi kuamuliwa kurudi makwao kasoro darasa la Saba ambao wanakabiliwa na mtihani wa kihitimu masomo yao septemba 7 na watakuwa wanajisaidia na walimu kwenye choo kimoja.

Akisoma barua ya kuifunga shule hiyo mbele ya wazazi na kamati ya shule afisa afya wa kata hiyo ya ndembezi Costancia Michael, alisema walifanya ukaguzi wa vyoo vya shule hiyo julai 12 mwaka huu wakati wanafunzi wakiwa rikizo nakukuta vyoo vya shule vikiwa katika hali mbaya huku vikianza kuanguka.

“Kwamujibu wa sheria ya afya ya mwaka 2009 kifungu cha 163 shule hii inapaswa kufungwa sababu ya vyoo vyake kuwa vibovu hali ambayo ni hatari kwa maisha ya wanafunzi na kuweza kusababisha vifo yakiwamo na magonjwa ya mlipuko kutokana na kujisaidia ovyo kwenye uzio wa shule hiyo,”alisema Michael.

Nao wazazi wanaosomesha watoto wao kwenye shule hiyo walikubaliana na uamuzi huo wa kufungwa kwa shule, huku wakiitupia lawama halmashauri kwa uzembe walioufanya wa kusimamia choo hicho kujengwa chini ya kiwango bila ya kuwekwa nondo chini yake na kusababisha kutitia na kuhatarisha maisha ya watoto wao.
Aidha wazazi hao waliitaka halmashauri ijenge vyoo hivyo haraka na wao hawawezi kuchangia chochote juu ya ujenzi huo, ikiwa hapo awali mwaka (20o4 ) walichanga fedha na hatimaye choo kujengwa chini ya kiwango kwa usimamizi wa halmashauri, hivyo wao ndio wenye jukumu la kujenga vyoo hivyo .

Naye mwalimu mkuu wa shule hiyo Nkulu Leostadias, alisema kufugwa kwa shule hiyo kutaathili taaluma ya wanafunzi ikiwa walikuwa wamejipanga kufundisha kwa bidii lakini alikishukuru wanafunzi wa darasa la Saba kubaki kuendelea na masomo kutokana na kukabiliwa na mtihani wa kuhitimu masomo yao.

Kwa upande wake Ofisa elimu wa shule za msingi wa halmashauri wa manispaa ya Shinyanga Yesse Kanyuma ambaye alihudhulia mkutano huo akimwakilisha mkurungezi Lewis Kalinjuna, alisema serikali imeshatenga Milioni 5 za kuanzia ujenzi wa vyoo hivyo, lakini wananchi wanapaswa kuchimba shimo ndio ujenzi uanze, kauli ambayo ilipingwa vikali na wazazi.

Na Marco Maduhu- Msukuma Blog


Powered by Blogger.