UWT SHINYANGA YACHANGIA DAMU SALAMA





SOMA HABARI KWA KINA
Umoja wa wanawake wa chama cha Mapinduzi Ccm (UWT) wilaya ya Shinyanga vijijini umechangia utoaji wa damu salama kwenye hospitali ya Rufaa ya mkoani hapa, kwa lengo la kuondoa vifo vya Mama na Mtoto vitokanavyo na uzazi sababu ya uhaba wa damu.
Hospitali hiyo ya Rufaa inakabiliwa na tatizo la uhaba wa damu asilimia 100 ikiwa bohari yake ina uniti 25 za damu salama, huku uhitaji ikiwa ni Uniti 20 kwa Siku moja, hali ambayo ni hatari hususani kwa akina mama wajawazito na watoto ambao ndio watumiaji wakubwa wa damu hiyo.
Akizungumza juzi wakati wakichangia damu hiyo salama Katibu wa umoja huo wa wanawake Grace Haule, alisema wameamua kufanya zoezi hilo ilikupunguza tatizo la uhaba wa damu salama kwenye hospitali hiyo ya rufaa, hali ambayo itaondoa ama kupunguza vifo vya mama na mtoto vitokanavyo na ukosefu wa damu mwilini.
Umoja wa wanawake wa chama cha Mapinduzi Ccm (UWT) wilaya ya Shinyanga vijijini umechangia utoaji wa damu salama kwenye hospitali ya Rufaa ya mkoani hapa, kwa lengo la kuondoa vifo vya Mama na Mtoto vitokanavyo na uzazi sababu ya uhaba wa damu.
Hospitali hiyo ya Rufaa inakabiliwa na tatizo la uhaba wa damu asilimia 100 ikiwa bohari yake ina uniti 25 za damu salama, huku uhitaji ikiwa ni Uniti 20 kwa Siku moja, hali ambayo ni hatari hususani kwa akina mama wajawazito na watoto ambao ndio watumiaji wakubwa wa damu hiyo.
Akizungumza juzi wakati wakichangia damu hiyo salama Katibu wa umoja huo wa wanawake Grace Haule, alisema wameamua kufanya zoezi hilo ilikupunguza tatizo la uhaba wa damu salama kwenye hospitali hiyo ya rufaa, hali ambayo itaondoa ama kupunguza vifo vya mama na mtoto vitokanavyo na ukosefu wa damu mwilini.
“Sisi umoja wa wanawake UWT Shinyanga vijijini tumeguswa na tatizo la uhaba wa damu salama kwenye hospitali ya Rufaa ya mkoa, na kufanikiwa kupata uniti 21 ambayo itasaidia kuokoa vifo vya wagonjwa wenye uhitaji wa damu,” alisema Haule
Naye kaimu mratibu wa Damu Salama kutoka Hospitali ya Rufaa mkoani humo Felix Manda aliupongeza umoja huo wa wanawake wa (CCM) Kwa moyo waliouonyesha wa kuchangia damu, ikiwa hospitali hiyo inakabiliwa na tatizo hilo kwa asilimia kubwa ambapo inatakiwa kwa wastani kuwe na Uniti 150 kwa wiki.
Aidha Mganga mkuu wa mkoa wa Shinyanga dk Ntuli Kapologwe alitoa takwimu za vifo vitokananavyo na uzazi kwa akina mama wajawazito, kuwa mwaka (2014) vilikuwa vifo 80 na (2015), vifo vilikuwa 60 huku akitoa wito kwa wananchi kuendelea kujitokeza kwa wingi kuchangia damu salama ilikumaliza vifo hivyo.
HABARI NA MARCO MADUHU MSUKUMA BLOG
Naye kaimu mratibu wa Damu Salama kutoka Hospitali ya Rufaa mkoani humo Felix Manda aliupongeza umoja huo wa wanawake wa (CCM) Kwa moyo waliouonyesha wa kuchangia damu, ikiwa hospitali hiyo inakabiliwa na tatizo hilo kwa asilimia kubwa ambapo inatakiwa kwa wastani kuwe na Uniti 150 kwa wiki.
Aidha Mganga mkuu wa mkoa wa Shinyanga dk Ntuli Kapologwe alitoa takwimu za vifo vitokananavyo na uzazi kwa akina mama wajawazito, kuwa mwaka (2014) vilikuwa vifo 80 na (2015), vifo vilikuwa 60 huku akitoa wito kwa wananchi kuendelea kujitokeza kwa wingi kuchangia damu salama ilikumaliza vifo hivyo.
HABARI NA MARCO MADUHU MSUKUMA BLOG