DC AINGIWA HOFU MWAKANI KUWEPO UHABA MKUBWA WA MADAWATI

Mkuu wa wilaya ya Shinyanga Josephine Matiro akizungumza mara baada ya kupokea madawati 50 kutoka kwenye Benki ya CRDB Tawi la mjini Shinyanga na kuwataka wananchi na wadau waendelee kujitokeza kuchangia madawati hayo ilikupata na yaziada endapo mwakani ikitokea idadi ya wanafunzi kuandikishwa ikizidi kusiwepo na uhaba huo tena Mashuleni na kusababisha wanafunzi kusoma wakiwa wamekaa chini.
Wakwanza kushoto ni Meneja wa Benki ya CRDB Said Pamui akishikana mkono na mkuu wa wilaya ya Shinyanga Josephine matiro kama ishara ya kumkabidhi madawati hayo 50 na mwenyesuti nyeus katika ni Meya wa manispaa ya shinyanga Gulaam Mukadam akifuatiwa na mkurugenzi wa halmshauri ya manispaa ya shinyanga Lewis Kalinjuna wakishuhudia zoezi hilo la kukabidhi madawati 50 yenye thamani ya Milioni 5.5


SOMA HABARI KAMILI

Mkuu wa wilaya ya shinyanga Josephine Matiro ameingiwa na hofu ya kuwepo na uhaba mkubwa wa madawati mashuleni mwaka 2017 kutokana na wananchi kuitikia suala la elimu bure na kupeleka watoto wao kwa wingi kupata elimu wakiwamo na wafungaji ambao walikuwa wakiipatia elimu kisogo.

Matiro ameingiwa na hofu hiyo kufuatia mwaka huu kuwepo na idadi kubwa ya wanafunzi mashuleni na kufanya baadhi ya shule kuwepo na uhaba mkubwa wa vyumba vya madarasa pamoja na uhaba  huo wa madawati huku serikali ikiendelea kuzitatua changamoto hizo moja baada ya nyingine.

Matiro alizungumza hayo  wakati akipokea madawati 50 yalitolewa na benki ya CRDB tawi la Shinyanga mjini kwa lengo la kuunga juhudi za serikali la kumaliza tatizo la uhaba wa madawati mashuleni, kuwa mwakani  ana hofu ya changamoto hiyo kuongezeka kutokana na wananchi kuitikia suala la elimu.

“Nimeingiwa na hofu kuwa mwakani kuna uwezekano wa tatizo la uhaba wa madawati mashuleni likawa kubwa zaidi kutokana na wananchi kuwa na muitikio mkubwa wa kupeleka watoto wao kupata elimu tofauti na miaka iliyopita,” alisema Matiro na kuongeza kuwa

“hivyo naomba wananchi na wadau wa maendeleo muendelee kuchangia utengenezaji wa madawati mashuleni, msichoke ilituweze kuwa na madawati ya ziada hata kama idadi ya wanafunzi ikiongezeka mwakani tatizo la wanafunzi kusoma wakiwa wamekaa chini liwe historia.”

Naye Meneja wa benki hiyo Said Pamui alisema madawati hayo 50 yamegharimu kiasi cha shilingi milioni 5.5 na wamekuwa na huduma ya kuchangia shughuli za maendeleo kwa wananchi kama kurudisha fadhira kwa wateja  huku akiahidi kuendelea kushirikiana na serikali kumaliza matatizo ndani ya jamii.

Kwa upande wake Ofisa Elimu ufundi wa halmashauri ya manispaa ya Shinyanga Mhela Mohamedi alisema awali kabla hawajapokea madawati hayo 50 kutoka benki ya CRDB walikuwa na upungufu wa madawati 1,969 lakini mpaka sasa wanakabiliwa na uhaba wa madawati 1,919

Na Marco Maduhu- Msukuma Blog.




Powered by Blogger.