WATU 30 WAHUKUMIWA KUNYONGWA MAUJI YA ALBINO,VIKONGWE

Waziri wa katiba na sheria Harrison Mwakyembe akizungumza na uongozi wa mkoa wa Shinyanga wakiwamo na Majaji na kuwataka wasimamie sheria vizuri kwa kuhudumia wananchi kwa kutenda haki, huku  akiutaka mkoa huo ukomeshe mauji ya albino na vikongwe ambayo yamelitia doa taifa, pamoja na kuwaagiza wakuu wa wilaya waunde kamati za maadili ambazo zitakwa zikihusika na kushughulikia malalamiko ya wananchi na kuyatatua kwa uharaka ili kuondoa manung'uniko kuwa serikali yao na vyombo vyake vya dola haviwatendei haki.


SOMA HABARI KAMILI

Waziri wa katiba na sheria Harrison Mwakyembe amesema jumla ya watuhumiwa 30 wa mauji ya vikongwe na albino hapa nchi wamehukumiwa kunyongwa baada ya kupatikana na hatia za kuusika na mauji ya watu hao wasio na hatia.

Mwakyembe amesema serikali itaendelea kutoa adhabu kali kwa watu ambao watabainika kuendelea kuhusika na mauji ya watu hao ilikuweza kumaliza tatizo hilo ambalo limeipaka matope nchi ya Tanzania kwa kuonekana sio kisiwa tena cha amani.

Mwakyembe ambaye pia ni Mbunge wa Kyela aliyabainisha hayo mjini Shinyanga wakati alipofanya ziara yake ya kikazi, kuwa kwa miaka ya hivi karibuni tatizo la mauji ya Albino na Vikongwe yamepungua hapa nchini, na watahakikisha wanayakomesha kwa kutoa adhabu kali kwa wauaji.

“Tatizo hili la mauji ya vikongwe na Albino linatutia sana doa nchi yetu kimataifa ambayo imekuwa ikisifika kwa amani na utulivu, hivyo natoa wito kwa wananchi waachane na mauji ya watu hawa wasio na hatia pamoja na Mahakama zifanye kazi kwa kutoa hukumu za haraka kwa watu watakao husika na mauji hayo,” alisema Mwakyembe.

Hata hivyo Mwakyembe alisema serikali itaanza mikakati ya kujenga Mahakama za mwanzo kwa kila Kata nchi nzima, ilikuondoa misongamano za kesi mahakamani pamoja na kukarabati majengo ya mahakama ambayo yamechakaa, sanjari na kuwataka wakuu wa wilaya waunde kamati za maadili za wilaya.

Aidha kwa upande wake mkuu wa mkoa wa Shinyanga Zainabu Telack, akisoma taarifa ya mkoa huo alitaja changamoto ambazo zinawakabili kuwa ni uchakavu wa majengo ya mahakama, uhaba wa mahakimu pamoja na magereza ya Shinyanga na Kahama kuwa finyu na hivyo kusababisha mrundikano wa wafungwa.

Na Marco Maduhu.Msukuma Blog







Powered by Blogger.