JAMII IMEONYWA KUGEUZA VITEGA UCHUMI WATOTO WA KIKE

Mkurugenzi wa Shirika la Agape John Myola akifungua kikao cha wadau watumiaji wa Mahakama mkoani Shinyanga juu ya kupanga mikakati ya kuzuia Mimba na Ndoa za utotoni pamoja na kubaini changamoto na kuzitatua dhidi ya kukomesha ukatili huo kwa watoto wadogo ,ambapo mradi huo unatekelezwa wilaya ya  Kishapu, Shinyanga vijijini na Manispaa

Wadua wa maendeleo mkoani Shinyanga wakiendelea kujadili namna ya kupambana na vitendo vya ukatiri mkoani Shinyanga hasa kukomesha ubakaji,ulawiti,mimba na ndoa za utotoni.

Wadau wa maendeleo wakiwa makini kusikiliza mikakati mbalimbali inayopangwa juu ya kukomesha matendo ya ukatiri mkoani Shinyanga ambayo inaongoza kwa aslimia 59. ikifuatiwa tabora 58 na mara 55.




SOMA HABARI KWA KINA

Wananchi mkoani  hapa  hususani wale wanaoishi maeneo ya vijijini, wameonywa kugeuza watoto wao wa kike vitega uchumi kwa kuwaodhesha wakiwa na umri mdogo huku wakiwakatisha masomo yao kwa tamaa ya kupata mali hasa mifugo, wametakiwa kuacha tabia hiyo ikiwa ni ukweukwaji wa haki ya mtoto.

Hayo yamezungumzwa na wadau wa maendeleo mkoani Shinyanga kwenye kikao cha kujadili namna ya kupanga mikakati ya kumaliza tatizo la mimba na ndoa za utotoni, ambapo mkoa huo unaongoza kwa asilimia 59,ikifuatiwa tabora 58, na yatatu ni mara 55.

Baadhi ya wadau hao David Nkulila na Maduhu Emmanuel wakizungumza kwenye kikao hicho kilicho andaliwa na Shirika la Agape linalotetea haki za watoto mkoani shinyanga, walisema tatizo ambalo limekuwa likisababisha vitendo hivyo kushika kasi ni jamii yenyewe kwa kugeuza watoto wa kike vitega uchumi.

“Tatizo hili la mimba na ndoa za utotoni kukithiri mkoani shinyanga linasababishwa na jamii yenyewe kwa kugeuza watoto wao wa kike vitega uchumi kwa kuwaodhesha kwa tamaa ya kupata mifugo mingi bila ya kujali anaumri mdogo wao wanacho thamini ni kupata mali,”alisema Nkulila

Aliongeza” ilikumaliza tatizo hili wananchi wapewe elimu ya kutosha juu ya madhara ya kuodhesha mtoto mdogo pamoja na kuwachukulia hatua kali za kisheria wazazi wenye tabia hiyo na kuwasweka rumande jambo ambalo litakuwa fundisho ikiwa jamii yetu imeshazoea mpaka mtu mmoja atolewe mfano.”

Hata hivyo wadau hao pia walivitaka vyombo vya maamuzi mkoani humo kuacha tabia ya kuchezea kesi hizo za mimba, ubakaji,ulawiti na ndoa za utotoni bali wanatakiwa kuwa kitu kimoja kwa kuzitolea hukumu haraka na kuwafunga watuhumiwa, kitendo ambacho kitakomesha ukatiri huo mkoani shinyanga.

Naye hakimu wa mahakama ya mwanzo kata ya usanda shinyanga vijijini Evalyn Polle, alisema kesi nyingi za namna hiyo wamekuwa wakishindwa kuzitolea hukumu kutokana na jamii yenyewe kulindana ambapo wamekuwa wakimalizana kimyakimya na hivyo mahakama kukosa ushahidi wa kutosha na kumwachia huru mtuhumiwa.

Kwa upande wake mkurugenzi wa shirika la Agape John Myola aliiomba serikali kushirikiana nao kikamilifu kupiga vita ukatili huo, kwakutoa maamuzi magumu hasa kwa viongozi wa ngazi za chini, vitongoji, mitaa na vijiji ambao ndio wamekuwa wakibariki vitendo hivyo kwa kuwalinda waharifu.


Na Marco Maduhu- Msukuma blog


Powered by Blogger.