MWALIMU MKUU MBARONI KWA KUMTEMBEZEA KICHAPO DIWANI

Diwani wa viti maalumu shinyanga vijijini Regina Charles akiwa amelazwa kwenye hospitali ya rufaa ya mkoa wa Shinyanga akipatiwa matibabu baada ya kutembezewa kichapo na Mwalimu mkuu wa shule ya msingi Itubabilo Paulo Mskabili baada ya kuhitalifiana kwenye kikao cha harusi.
Diwani wa viti maalumu Regina Charels akipatiwa matibabu hospitali ya Rufaa mkoani Shinyanga, ambapo pia alipewa rufaa ya kwenda Bugando jijini Mwanza kupatiwa matibabu zaidi.
Mkurugenzi wa halmashauri ya shinyanga vijijini Kiomon Kibamba akimsalimia diwani katika hospitali ya rufaa ya mkoa


SOMA HABARI KWA KINA.

Jeshi la Polisi mkoani shinyanga lina mshikilia mwalimu mkuu wa shule ya msingi Itubamilo shinyanga vijijini  Paulo Msakabili, kwa  tuhuma za kumshambulia diwani viti maalumu Mengi Charles mara baada kutofautia kauli kwenye kikao cha harusi.

Tukio hilo limetokea juzi ambapo diwani huyo alikuwa na mwalimu mkuu  kwenye kikao cha harusi na wajumbe wengine wa kamati tendaji wakijadili mikakati ya kufanikisha harusi ya ndugu yao ambapo mkuu huyo wa shule alitaka kamati ya mapambo apewe yeye lakini diwani alipinga na uhasama ukaanzia hapo.

Akielezea tukio hilo kwa shida huku akiwa amelezwa kwenye hospitali ya rufaa ya mkoa wa shinyanga diwani Chalres alisema baada ya kikao hicho cha harusi kuisha ndipo mwalimu huyo alipomfuata na kumkata mtama na kuanza kumshambulia sehemu za kichwani na kumsababishia maumivu makali na kuharibu jicho lake la kushoto.

“Ugomvi uliibuka pale nilipopinga mwalimu huyo kupewa kamati ya mapambo ambapo alidai kunamtu anamfahamu ampe na kumtaka aje na huyo mpambaji iliwajumbe wa kamati tendaji wamuone na kumuhoji pamoja na kufahamu gharama zake lakini Mwalimu huyo alikuja juu na kuanza kunishambulia,”alisema  Charles

Aidha kaimu mganga mfawidhi wa hospitali ya rufaa mkoani shinyanga dkt Mwita Ngutunya alikiri kumpokea  diwani huyo na kudai kuwa hali yake ni mbaya hasa kwenye jicho lake la kushoto na taya ambapo wamempatia rufaa ya kwenda kutibiwa bugando jijini mwanza kwa matibabu zaidi.

Kwa upande wake kaimu kamanda wa jeshi la polisi mkoani shinyanga Graifton Mushi alithibitisha kutokea kwa tukio hilo na mtuhumiwa wanamshikilia na upelelezi ukikiamilika na kubainika anakosa atafikishwa mahakamani kujibu shitaka la kushambulia mwili.

Na Marco Maduhu- Msukuma Blog

   


Powered by Blogger.