ZITTO AWATAKA WANACHAMA WA ACT WAZALENDO KUJIANDAA KISAIKOLOJIA UCHAGUZI MKUU 2020

Kiongozi wa chama cha Act wazalendo Taifa Zitto Kabwe, amewataka wanachama wa chama hicho kujiandaa kisaikolojia katika chaguzi zijazo za viongozi wa Serikali za mitaa (2019) pamoja na uchaguzi mkuu (2020), kutokana na siasa zinavyoendeshwa hivi sasa kwa kubinywa kwa uhuru wa demokrasia.

Alisema siasa za sasa hivi Tanzania ni ngumu, hivyo wasikate tamaa kuendeleza mapambano ya kupigania demokrasia hapa nchini, pamoja na kuendelea kuulinda mfumo wa vyama vingi ambao ndio mkombozi kwa watanzania, na waendelee kujipanga kugombea majimbo katika chaguzi hizo ukiwamo mkuu wa 2020.

Alisema kutokana na jambo hilo la kubinywa kwa demokrasia hapa nchini, hivyo waanze kujiandaa kisaikolojia kwenye chaguzi hizo na kutotishika na watu wanaohama vyama vya siasa, bali waanze kujipanga mapema namna ya kulinda wizi wa kura, kutafuta mawakala waaminifu, pamoja na viongozi kutatua kero za wananchi.

Zitto aliyabainisha hayo leo Februari 28 mjini Shinyanga alipokuwa  kwenye ziara yake ya kuimarisha Chama alipokutana kuzungumza na viongozi pamoja na wanachama wa chama hicho mjini humo, kuwa wasiteteleka na uendeshwaji wa siasa hapa nchini na kuanza kuhama vyama hovyo, bali wajipange kisaikolojia na kukijenga chama.

“Tunataka chama chetu kiwe tofauti na vyama vingine vya upinzani kuto hama hama vyama kwa kuhofia uchaguzi mkuu ujao kuwa hawatopata kura wala uongozi, bali sisi tujipange kisaikolojia na kufanya kazi ya kusikiliza na kutatua kero za wananchi, ambao ndio wenye ridhaa ya kutupatia uongozi,”alisema.

Aliongeza kwa kuwataka viongozi wa chama hicho ambao walipewa ridhaa ya wananchi kwenye chaguzi zilizopita (2014-15) za madiwani na ubunge wawatumikie wananchi ipasavyo kwa kutatua kero zao, ili kuonyesha utofauti wa viongozi wa ACT na wa vyama vingine, ilikuendelea kukiimarisha chama kwa wananchi.

Nao baadhi ya wanachama hao akiwamo Maarufu Hassani, walionyesha wasiwasi juu ya baadhi ya viongozi ambao walipata ridhaa kwenye chaguzi zilizopita (2014-15), kuwa kutokana na vuguvugu la kisiasa hapa nchini la kubinywa kwa demokrasia na chaguzi zinavyoendeshwa, kuwa kuna uwezekano wa viongozi  hao wasirudi 2020.

Pia katika ziara hiyo, Zitto alifanikiwa kuvuna wanachama wapya Tisa kutoka vyama mbalimbali vya siasa, pamoja na kuwapatia kiapo cha utii wa chama hicho, ilikuendelea kukilinda na kukijenga chama kwa wananchi, ambao ndio watawapatia ridhaa ya kushika nchi.


TAZAMA HABARI PICHA HAPA CHINI

 Katibu wa Jimbo wa chama cha ACT Wazalendo mjini Shinyanga Merkyoli Tafuta, akimkaribisha Kiongozi huyo wa kitaifa Zitto Kabwe, pamoja na kuwatambulisha viongozi mbalimbali wa Chama hicho mkoani Shinyanga na baadhi ya wanachama ambao walihudhulia kikao cha kiongozi huyo ambacho kililenga kuimarisha chama..
 Zitto Kabwe ambaye pia ni mbunge wa jimbo la Kigoma mjini ,akiwatoa wasiwasi wanachama wa ACT Wazalendo kuwa nchi hii haiwezi kurudi kwenye mfumo wa chama kimoja licha ya nguvu nyingi kutumika ya kuuwa upinzani, bali kinachopaswa ni kusimama imara na kupigania demokrasia ya kweli, ambayo itawafanya watu kuwa huru na kufanya kile wanachokitaka bila ya kuvunja sheria za nchini, na kuwaasa pia viongozi wa chama hicho waliopewa ridhaa ya kuongoza na wananchi (2014-15) wajitume kufanya kazi ya kutatua kero za wananchi, ili kuonyesha utofauti kati ya viongozi wa ACT na vyama vingine.
 Mjumbe wa Kamati kuu ya Chama hicho Taifa  Nyangaki Shilungushela, akizungumza kwenye kikao hicho aliwataka  wanachama hao wa ACT Wazalendo, kuendelea kujiamini na kufanya kazi licha ya chama chao kubezwa kuwa ni Kichanga na CCM "B" bali wao wasiangalie propaganda za wakosaji ikiwa chama hicho kwa sasa ndio mpinzani wa kweli na ndio kina aminiwa na wananchi katika kuwaletea ukombozi.
 Wanachama wa ACT Wazalendo wakiwa kwenye kikao cha kiongozi wao wa chama hicho Taifa ZittoKabwe, na kuaswa kuendelea kukijenga chama na kutoteteleka na siasa za ubinywaji wa demokrasia ambazo zinaendeshwa hapa nchini.
 Wanachama wa ACT Wazalendo wakiendelea na kikoa cha kiongozi wao wa kitaifa Zitto Kabwe.
 Wanachama wa ACT Wazalendo wakiwa kwenye kikao wakisikiliza ujumbe mbalimbali kutoka kwa kiongozi wao wa chama hicho taifa Zitto Kabwe.
 Kikao kikiendelea.
 Mwenyekiti wa ACT Wazalendo mkoa wa Shinyanga Siri Yasini, akimkaribisha kiongozi wa chama hicho Taifa Zuberi Kabwe, kupokea wanachama wapya Tisa ambao wanajiunga na chama kutoka vyama mbalimbali vya siasa.
 Kiongozi wa chama hicho Taifa Zitto Kabwe, akimpatia kadi ya chama hicho Mwanachama mpya Ester Mtupili ambaye alikuwa Mwanachama wa Chadema.
 Kiongozi wa chama cha ACT Wazalendo Zitto Kabwe akiwaapisha kiapo cha utii wanachama wapya Tisa waliojiunga na chama hicho wakitokea vyama mbalimbali vya kisiasa.
 Zitto Kabwe akiwataka wanachama wapya na wazamani kuungana kwa pamoja kukijenga chama, na kuachana na siasa za malumbano, bali wajikite kukipigania chama ilikuendelea kuaminiwa na wananchi ambao ndio wenye ridhaa ya kuwapatia viongozi wengi kwenye chaguzi zijazo ukiwamo uchaguzi mkuu 2020, kwa kuwapatia madiwani wengi ,wenyeviti, na wabunge na hata kushika dola.
Wanachama wa ACT Wazalendo wakipiga picha ya pamoja na kiongozi wao wa chama hicho Taifa Zitto Kabwe.

Na Marco Maduhu, ambaye pia ni Mwandishi wa Gazeti la Nipashe, habari hizi pia utazipata kupitia gazeti la NIPASHE .













Powered by Blogger.